Header Ads

Jiji la Dar es Salaam Kufumuliwa na Kupangwa Upya


Waziri wa Nyumba, Ardhi na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi amesema Jiji la Dar es Salaam litafumuliwa na kupangwa upya baada ya Ramani ya Mipango Miji (Master Plan) mpya kukamilika.

Pia, amesema Serikali ipo kwenye mkakati wa kuhakikisha ndani ya miaka 10 ijayo, ardhi yote nchini itakuwa imekamilika kupimwa na kupangwa kwa matumizi mbalimbali. 

Akizungumza na wadau wa Sekta ya Uendelezaji Ujenzi Dar es Salaam jana, Waziri Lukuvi alisema Jiji la Dar es Salaam linaongoza kwa ubovu wa upangaji miji. 

Alisema kwa sababu hiyo, ameagiza kuandaliwa kwa Mpango Mji Mpya ambao utakamilika Julai, baada ya ule wa awali kuoneakana mbovu. 

“Mwanzo hatukufanya vizuri. Tuliajiri Consultant (mshauri) wa Master Plan (Mipango Miji) kutoka Italia sitaki kumtaja na yule Mswahili na wengine walioshirikiana nao, lakini kwa ufupi walifanya vibaya. Fedha imekwisha lakini kazi siyo nzuri,” alisema. 

No comments