Header Ads

Samaki wa milioni 20/- wakamatwa Sumbawanga.


IDARA ya Uvuvi na Mifugo, Hamashauri ya Wilaya ya Sumbawanga mkoani Rukwa imekamata shehena ya samaki wabichi na wakavu wenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 20.
Shehena hiyo ya samaki inadaiwa kuvuliwa kwa kutumia nyavu haramu za kuvulia samaki ambazo zimepigwa marufuku kuvulia katika Ziwa Rukwa wilayani Sumbawanga ambayo ilikuwa ikisafirishwa kwenda nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kupitia mji mdogo wa Tunduma mkoani Mbeya .
Akizungumza na gazeti hili Ofisa Uvuvi na Mifugo wa Halmashauri ya wilaya ya Sumbawanga , Denis Maghala alisema baadhi ya wavuvi wanaendelea kuvua katika Ziwa Rukwa licha ya kufungwa kwake kwa miezi mitatu hadi Machi 31 mwaka huu.
“Wavuvi hao wanavua ziwani kwa njia ya haramu na kuwauzia samaki wabichi na wakavu kwa wafanyabiashara ambao husafirisha kwa kutumia magari makubwa kwenda jijini Mbeya pia nchi jirani ya DRC,” alisema.
Alisema kuwa idara yake imekuwa ikifanya doria za mara kwa mara ambapo Januari 29 mwaka huu gari aina ya Fuso lenye nambari za usajiri T910 ARL mali ya Selemani Jimmy lilikamatwa likiwa na shehena ya samaki wabichi na wakavu wenye thamani ya mamilioni.
CHANZO:HABARI LEO

No comments