Header Ads

MUGABE ATUMIA MANENO MAKALI KUMJIBU TRUMP.



Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe ameamua kumjibu mgombea urais wa Marekani, Donald Trump ambaye hivi karibuni alidai kuwa akiingia madarakani atahakikisha anawakamata na kuwafunga yeye na rais mwenzake wa Uganda, Yoweri Museveni.
Mugabe alitumia hafla ya kuchangisha fedha kwa ajili ya maendeleo iliyofanyika jijini Harare juzi (Januari 3) kumjibu Trump. Alisema kuwa Trump ana damu ya Hitler.
Hivi ndivyo alivyoeleza:
“Hivi karibuni yule mwendawazimu anayetaka kuwa rais wa Marekani alisema kuwa atawakamata baadhi ya marais wa Afrika akiwemo kaka yangu Yoweri na mimi na kutufunga gerezani endapo atakuwa rais.

“Naomba nimueleze hapa kwamba Trump hataweza kutupeleka popote kwa sababu sisi waafrika ni imara zaidi duniani na hatuogopi. Ningependa kila mmoja kufahamu kuwa sina cha kuogopa na nataka niiambie dunia kuwa huyo mzimu wa Hitler umemchukua na anakaribia kufanya ya hovyo watu wa Marekani wakimchagua.

“Kama ambavyo babu yake Hitler alivyosababisha vita ya pili ya dunia, na yeye anataka kuanzisha vita ya tatu ya dunia ili aache kumbukumbu lakini dunia haitaruhusu hilo.
Hivi inakuaje unaanza hata kufikiria kuwa utamkamata mtu kama mimi? Hivi kichwa cha Trump kiko sawa? Na… hivi kuna madaktari wa kutosha Marekani kumpima ukichaa huyu mtu?

Haya ni baadhi ya maneno aliyoyazungumza Trump wakati wa kampeni zake;
“I want to reiterate here before America’s greatest heroes that I will not condone any dictatorial tendencies exhibited by dictators around the world especially the two old men from Zimbabwe and Uganda”
Mugabe and Museveni must be put on notice that their days are numbered and that I am going to arrest them and lock them in prison. If the past American administrations have failed to stop these two despots, I will personally do it”
Mugabe and Museveni have given the world enough troubles and its about time someone puts to an end all these madness for peace to prevail” .
If Obama fears them, I will never fear them. If clinton and Bush feared them, If the Pope kneels before them, I will never be reduced to that level. I will never be cowed. I promise to clean all the political mess around the world and promote international justice” 

No comments