Header Ads

WHO:CUBA HAINA KASWENDE, UKIMWI KWA WATOTO.

Dr Carissa Etienne, ambaye amekuwa akishirikiana na WHO akitangaza ufanisi wa Cuba
Shirika la afya duniani WHO, limethibitisha kuwa Cuba imemaliza kabisa maambukizi ya ukimwi kutoka kwa mama mzazi na Kaswende.
Mkuu wa shirika hilo WHO, Daktari Margaret Chan, ametaja ufanisi huo kuwa ''ni mkubwa zaidi kuwahi kutokea kwa afya ya umma.''
Mafanikio hayo ya kutajika yanafuatia kampeini ya muda mrefu miongoni mwa wanawake waja wazito ambao wamekuwa wakishauriwa kuanza kupokea matibabu mapema na kufanyiwa vipimo mahsusi ilikujua hali ya afya ya mama na mwanaye .
WHO inatumai kuwa mafanikio hayo ya Cuba yataigwa na mataifa mengine.
Kwa mujibu wa takwimu za WHO, Kila mwaka takriban wanawake milioni moja nukta nne (1.4) i walioambukizwa virusi vya ukimwi duniani, hupata uja uzito.
Iwapo hawapokei matibabu mapema asilimia 15-45% ya wanawake hao huwaambukiza watoto wanaojifungua wakati wa kujifungua na pia kupitia kwa maziwa ya mama.
Hatari ya maambukizi hupungua kwa kiasi kikubwa na kufikia asilimia moja pekee 1% baada ya kupokea madawa ya kupunguza makali ya ugonjwa wa Ukimwi.
Aidha wanawake wengine milioni moja huambukizwa kaswende wakiwa wajawazito kila mwaka.
Iwapo wanawake hao watapokea matibabu mapema wanaweza kuzuia kuwaambukiza watoto wao.
null
Kote duniani wanawake waja wazito 7 kati ya 10 ambao wameambukizwa ukimwi hupokea,madawa ya kupunguza makali ya ukimwi
Nchini Cuba, chini ya asilimia 2% ya watoto huzaliwa na maambukizi ya maradhi hayo.
Hii ikiwa ni kiwango cha chini mno kinachoweza kufikiwa kufuatia matibabu.
Kote duniani wanawake 7 kati ya 10 ambao wameambukizwa ukimwi hupokea,madawa ya kupunguza makali ya ukimwi ilikuzuia maambukizi kwa watoto watakaojifungua.
Dr Carissa Etienne, ambaye amekuwa akishirikiana na WHO amesema kuwa mafanikio ya Cuba yanapaswa kuigwa kote duniani ilikupunguza au hata kumaliza kabisa maambukizi ya Ukimwi na kaswende kutoka kwa mama mja mzito kwa mwanawe.BBC

No comments