Header Ads

UINGEREZA NJE YA KOMBE LA DUNIA WANAWAKE.

Timu ya taifa ya wanawake ya England imetupwa nje ya michuano ya kombe la dunia la wanawake kwenye mchezo wa nusu fainali kwa kichapo cha goli 2-1 kutoka kwa Japan ambao ndio mabingwa watetezi wa kombe hilo kwenye michuano inayoendelea huko nchini Canada.
Japani walikuwa wakwanza kupata goli la kwanza dakika ya 33 kupitia kwa nahodha wao Aya Miyama baada ya Claire Rafferty kumfanyia madhambi Saori Ariyoshi nje kidogo ya eneo la hatari lakini mwamuzi akaamuru ipigwe penati na Miyami akaukwamisha mpira kambani.MJENGWA.

No comments