Header Ads

DK. SLAA KURUDI CCM?


Image result for DK.SLAA

Hali ya kisiasa nchini inazidi kuwa tete, kufuatia hatua ya Chadema kukiuza Chama hicho kwa Waziri Mkuu aliyelazimishwa kujiuzulu kwa kashfa ya ufisadi wa kampuni ya Richmond, Edward Lowassa. 

Image result for lowassa


Makubaliano ya Chadema kumuuzia Lowassa Chama hicho yamefanywa Jumapili iliyopita kati ya Mwenyekiti wa Chama hicho Freeman Mbowe na Lowassa ambapo Lowassa alikubali kutoa shilingi Bilioni kumi taslim ili aweze kutimiza safari yake ya matumaini ya kugombea Urais kwa tiketi ya Chama hicho, baada ya jina lake kukatwa na CCM, kwasababu ya makandokando ya Ufisadi yanayomkabili. 


Hatua ya Mbowe kukiuza Chama hicho kwa Lowassa imemkera mno Katibu Mkuu wa Chama hicho, Dk. Wilibrod Slaa. Sababu kubwa ya Dk. Slaa kupinga Lowassa kupokelewa Chadema na kuuziwa chama hicho ili aweze kugombea Urais, ni imani kubwa aliyonayo kwamba Lowassa ni Fisadi mkubwa ambaye alistahili kuwa Gerezani au kunyongwa, badala ya kupewa heshima ya kugombea Urais katika Chama hicho. 


"Kama Lowassa huyu huyu amekatwa na CCM kutokana na ufisadi wake, vipi leo aonekane ni msafi ndani ya Chadema?!", amenukuliwa akihoji na kulalamika Dk. Slaa. 


Kutokana na kinyongo hicho alichonacho Dk. Slaa dhidi ya Mwenyekiti wake Mbowe kwa kukiuza chama hicho kwa Lowassa, duru za kisiasa nchini zimebainisha kuwa Dk. Slaa mapema wiki ijayo atafanya maamuzi magumu ya kukihama chama hicho Ili kuachana kabisa na siasa au ikibidi kurejea katika chama chake cha zamani cha CCM. 


"Kamwe siwezi kukaa meza moja na Fisadi Lowassa ambaye nilimtangaza kwa kinywa changu mwenyewe katika list of shame pale Mwembeyanga. Ni afadhali hata niachane kabisa na Siasa na ikibidi nirudi katika kazi yangu ya Kanisa kuliko kukaa meza moja na Mafisadi", amenukuliwa akiapa kwa uchungu mkubwa Dk. Slaa ambaye anasifika mno kwa ukali wake wa mapambano dhidi ya Mafisadi hapa nchini. 


SOURCE: MWANAHALISI FORUM 27.07.2015

No comments