Header Ads

WAKAZI WA GEITA WAHIMIZWA KUTUMIA CHUO KIKUU HURIA KUKUZA KIWANGO CHAO CHA ELIMU.

Mkuu wa chuo kikuu huria Nchini,ambaye ni waziri Mkuu mstaafu Mizengo Pinda akizungumza na watumishi wa serikali Mkoa wa Geita pamoja na kamati ya ulinzi na usalama baada ya kuwasili Mkoani Geita.

Mkuu wa chuo kikuu huria Nchini,ambaye ni waziri Mkuu mstaafu Mizengo Pinda akiwa kwenye picha ya pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Geita pamoja na  Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), Profesa Elifas Bisanda na watumishi wa serikali pamoja na kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa.

Mkuu wa chuo kikuu huria Nchini,ambaye ni waziri Mkuu mstaafu Mizengo Pinda akisalimiana na baadhi ya wanafunzi wa tawi la Geita wakati alipowasili kwenye chuo hicho.

Mkuu wa chuo kikuu huria Nchini,ambaye ni waziri Mkuu mstaafu Mizengo Pinda,akimsikiliza Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), Profesa Elifas Bisanda wakati alipokuwa akizungumza na wanafunzi wa chuo hicho.

Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), Profesa Elifas Bisanda akizungumza na wanafunzi wa chuo hicho tawi la Geita kwenye ukumbi wa mikutano wa halmashauri ya wilaya hiyo.

Mkurugenzi wa chuo kikuu huria tawi la Geita,Ally Abdul akitoa taarifa ya namna chuo hicho kilivyo anza hadi kilipo kwa sasa.

Mkurugenzi wa chuo kikuu huria tawi la Geita,Ally Abdul  akimpatia zawadi Mkuu wa chuo kikuu huria Nchini,ambaye ni waziri Mkuu mstaafu Mizengo Pinda.
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), Profesa Elifas Bisanda  pamoja na Mkuu wa chuo kikuu huria Nchini,ambaye ni waziri Mkuu mstaafu Mizengo Pinda wakionesha zawadi ambazo wamepatiwa.

Mkuu wa mkoa wa Geita,Mhandisi Robert Luhumbi akielezea umuhimu wa chuo hicho katika Mkoa wa Geita.

Mkuu wa chuo kikuu huria Nchini,ambaye ni waziri Mkuu mstaafu Mizengo Pinda akizungumza na wanafunzi wa chuo hicho tawi la Geita.

Mkuu wa chuo kikuu huria Nchini,ambaye ni waziri Mkuu mstaafu Mizengo Pinda,akiagana na mkuu wa mkoa wa Geita,Mhandisi Robert Luhumbi nje ya ukumbi wa mikutano wa halmashauri ya Wilaya ya Geita.
Na,Joel Maduka,Geita.


Wananchi na watumishi pamoja na wale ambao wanafanya kazi sekta binafisi mkoani Geita,wametakiwa kutumia fursa ya chuo kikuu huria ili kuongeza kiwango cha  elimu pamoja na maarifa ambayo yatawasaidia kwenye shughuli zao za kila siku.

Wito huo umetolewa na Waziri Mkuu mstaafu,ambaye ni Mkuu wa chuo kikuu huria nchini,Mizengo Pinda wakati wa ziara yake ya kutembelea na kujionea shughuli ambazo zinafanywa na chuo hicho mkoani humo pamoja na kuzungumza na wanafunzi.



Mh,Pinda alisema ni vyema kwa  wakuu wa mikoa  kuendelea kuhamasisha  watumishi ambao wapo kazini kujiongezea uwezo zaidi kielimu kwenye vyuo vikuu huria ili kufikia adhima ya Tanzania ya viwanda ifikapo 2025.


“Mkuu wa mkoa na katibu tawala tusaidieni sana kuhamasisha kundi la watalaamu ambao wapo serikalini kutumia fursa hii kujiongezea uwezo ili waweze kuwa kwenye nafasi nzuri zaidi ya kielimu”Alisisitiza  Pinda.

Naye mkuu wa mkoa wa Geita,Mhandisi Robert Luhumbi alisema suala la elimu halina mwisho kwani  pindi unavyozidi kuongeza elimu ndio unafungua mianya ya kukabiliana na janga la umasikini.



“Elimu haina mwisho jinsi ambavyo unachukua nafasi ya kupata elimu unapata uwezo wa kupigana vita vya umasikini vita vya kuondoka kiwango ulichopo kwenda kwenye kiwango cha juu hivyo basi natoa wito kwa wananchi wote waliopo mkoa wa Geita kutumia fursa hii kujiendeleza kielimu kwenye chuo hiki huria”Alisema Luhumbi.

Hata hivyo  mkurugenzi wa chuo kikuu huria tawi la Geita,Ally Abdul,ameishukuru serikali kwa kuwapatia hati miliki ya kiwanja kwa ajili ya kuongeza majengo pamoja na msaada wa vitabu 285.

Chuo kikuu huria Tawi la Geita kilianza  mwaka 2012 na kufanya kazi rasmi mwaka 2013 kikiwa na takribani   wanafunzi 74 na wengi kati ya hao walisajiliwa kutoka  Mwanza wakati  huo Geita ikiwa ni wilaya idadi ya wanafunzi iliongezeka kwa mwaka 2014 na 2015 kufikia   118 na mwaka huu kuna jumla ya wanafunzi ni 285.

No comments