Header Ads

Mtanzania akamatwa na kilo 32 za dhahabu Kenya


MAMLAKA ya Mapato Kenya (KRA) imesema, imemkamata raia wa Tanzania akiwa na kilo 32.25 za dhahabu zenye thamani ya shilingi milioni 100 za nchi hiyo ambazo ni sawa na takribani shilingi bilioni mbili za Tanzania.
Taarifa ya KRA imesema, mtuhumiwa huyo alikamatwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta (JKIA) akiwa na miche ya dhahabu.
Kwa mujibu wa KRA, Mtanzania huyo mwenye umri wa miaka 46 alikutwa na gramu 32,255.50 za madini hayo na hati ya malipo ya Dola za Marekani 859,890.
Taarifa ya KRA imeeleza kwa, kijana huyo alifika JKIA Ijumaa Februari 16 saa 9.05 alasiri kwa ndege ya shirika la Precision, alitoka Mwanza akapita Kilimanjaro na alikuwa anakwenda Dubai kwa ndege ya Shirika la Ndege la Kenya, Kenya Airways.
Kwa mujibu wa mamlaka hiyo, usafirishaji bidhaa kwa siri vikiwemo vito vya thamani ni kinyume cha kifungu cha 85 (3) cha Sheria ya Usimamizi wa Forodha ya mwaka 2004 ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Upelelezi kuhuus dhahabu iliyokamatwa unaendelea na sasa ipo chini ya KRA na mamlaka za usimamizi wa forodha za mipaka.
SOURCE:HABARILEO

No comments