Header Ads

MGODI WA GGM WAPEWA SIKU 2 KUANZA MCHAKATO KUWAFIDIA WANANCHI.

Naibu  waziri  wa madini Stanlaus Nyongo Akizungumza na  Wakazi  Wa Kijiji Cha Nyakabale  wakati wa ziara yake Mkoani Geita.


Naibu  waziri  wa madini Stanlaus Nyongo akishiriki zoezi la kuponda mawe ya dhahabu.

Naibu  waziri  wa madini Stanlaus Nyongo akizungumza na diwani wa kata ya Mgusu Pastory Ruhusa.

Naibu Waziri  Akimsikiliza Pili Mwaluko Anaefanya Kazi Ya Uchenjuaji Madini kwenye mtaa wa Nyakabale. 

Wananchi wakiwa kwenye Mkutano wa pamoja na Naibu Waziri  wa madini Stanlaus Nyongo.

Na,Joel Maduka,Geita.


Naibu  waziri wa madini  Stanslaus Nyongo amesema kuwa serikali ya awamu ya tano haiko tayari  kuona mtu akilalamika ,kunyanyaswa ama kunyimwa haki yake.

Kauli hiyo ameitoa wakati akiongea na wananchi wa kijiji cha Nyakabale  kata ya  Mgusu  Wilayani Geita wakati wa ziara yake ya siku mbili Mkoani humo ya kuzungukia maeneo ya uchimbaji pamoja na kusikiliza kero za wananchi ambao wanazunguka kwenye baadhi ya maeneo ya mgodi wa Geita(GGM).

Hatua  hiyo ya Naibu Waziri Nyongo imekuja baada ya kusikia malalamiko mengi kutoka kwa wananchi juu ya mgodi wa GGM kushindwa kuwalipa fidia kwa muda mrefu pamoja na kuwepo kwa maagizo mengi ambayo yamekuwa yakitolewa na baadhi ya viongozi ambao wamekuwa wakifika Mkoani humo.

 “Tukikaa kwenye viyoyozi hatuambiwi ukweli na wamiliki wa migodi lakini tunapo fika katika eneo husika tunapata ukweli , unakuta mtu kazaliwa hapo kakulia hapo amejenga ana watoto halafu mtu anakuondoa kwa madai kuwa upo kwenye leseni yake  hainiingii akilini kama unahitaji eneo langu njoo tukae tumalizane  unipe changu mimi nisepe inakuwa nilipe nisepe ”alisema Nyongo.

Hata hivyo aliwataka watu wa mgodi huo kuwalipa wananchi hao ama waondoke wawaachie wananchi hao eneo lao waendelee kuchimba na sio kuwazuia ikiwa hawafanyi shughuli za uchimbaji kwa sasa .

Awali Akitoa malalamiko kwa Naibu waziri  mwananchi wa Nyakabale kwa niaba ya wenzake Joseph Kihengu alimwambia Naibu waziri  kuwa wanailaumu serikali iliyopita  inawezekana wakati wanabinafsisha mgodi huu na wao walibinafsishwa humo bila kujua.

“Mheshimiwa   kipindi cha nyuma usingeweza kupata umati kama huu, umati huu umetokana na imani ya serikali ya awamu ya tano waliyo nayo hivyo serikali iwaangalie kwa jicho la tatu ili watu wa Nyakabale  wajue hatima ya maeneo ambayo yapo ndani ya bikoni za mgodi wa GGM”Alisema Joseph.


No comments