Header Ads

MAHUJAJI WANNE WAREJEA SALAMA MKOANI GEITA

PICHA NA MAELEZO:MADUKA ONLINE
Alhaji Said Kalidushi akisalimiana na wapendwa ambao alikutana nao katika kivuko cha Busisi jijini M,wanza wakati alipokuwa akitokea Uwanja wa ndege wa Jijini Mwanza.

Ndugu, jamaa,marafiki na waumini wa dini ya Kiislamu wakiwa na furaha kubwa baada ya kukutana na wapendwa wao.Alhad Khamisi Mrisho Mlea akisalimiana na baadhi ya waumini.

Furaha ndipo ilipoongezeka baada ya kumuona shehe Mkuu wa Mkoa wa Geita Alhadi Yusufu Kabaju.

Wakielekea katika usafiri kwa ajili ya safari ya kuelekea Geita baada ya kuwa wamesalimiana na wapendwa wao wakitokea jijini Mwanza.

Burudani na shangwe pia vilirindima katika mapokezi hayo.

Shekhe Mkuu akiwa amewasili Mkoani Geita baada ya safari ndefu.



Akina mama wakiimba nyimbo za shangwe na nderemo za kuwashangilia mahujaji ambao wametokea makkah.




Shekhe Yusufu, akiwaeleza waumini namna ambavyo wanatakiwa kuendelea kumcha Mungu na mwisho wa siku ni vyema wakafika katika Nchi ya Saud Arabia kwaajili ya kuhiji.

Waumini wakimsikiliza  kwa makini shekhe wakati wa ibada ya shukrani.

GEITA:Mahujaji wanne wakiongozwa na Shekhe  Mkuu wa Mkoa wa Geita,Alhadi Yusufu Kabaju,wamerejea mkoani humo  wakitokea nchini Saud Arabia  ambako walikwenda  kuhiji ikiwa ni moja kati ya nguzo muhimu katika Dini ya Kiislamu.

Akizungumza katika ibada ya kumshukuru Mungu kuwarudisha salama,shehe Alhadi Yusufu Kabaju,amesema kuwa ni jambo la busara sana kumshukuru Mungu  kwani amewasaidia katika safari yao kwenda na kurudi salama.

“Ni jambo la kumshukuru  mwenyezi Mungu sana na Mtume wake Muhammad (SAW)  ni jambo ambalo waislamu tunapaswa kumshuru mwenyezi Mungu sana ,safari ya kiibada ni safari nzito sana kwasababu ukiangalia safari ya kwenda na kurudi ni safari nzito sana huwezi ukaamini kuwa mtu anaweza kwenda safari hiyo na umma wa Dunia nzima mkakutana sehemu moja.”alisema Shehe Kabaju.

Aidha kwa upande wao wahumini wa dini ya kislamu wameshukuru na pia wamefurahia kwa kurudi salama kwa mahujaji ambao walikwenda kuhiji Makkah.

Mahujaji hao  wamerejea siku ya Jumamosi wakitokea nchini Saudi Arabia ambako walikwenda kuhiji.
Imeandaliwa na Joel Maduka.

No comments