WACHUNGAJI WAWILI NA MSHIRIKA WAFARIKI KATIKA AJALI YA GARI.
Askofu mkuu wa kanisa la FPCT nchini David Batenzi.
Wachungaji
wawili wa kanisa la FPCT, na mshirika mmoja wamefariki na wengine wanne
kujeruhiwa katika ajali ya gari aneo la Mabama wilayani Uyui walipokuwa
wakisafiri kutoka Mishamo wilayani Mpanda mkoani Katavi, wakielekea jijini
Mwanza katika mazishi ya mchungaji wao kiongozi.
Akiongea na waandishi wa habari katika hospitali ya
rufaa ya mkoa wa Tabora Kitete, mchungaji Banyiyezako Selestini (majeruhi),
amewataja marehemu kwa majina ya Mchungaji Ndezimana Sefania, na mchungaji Pili
Simion, na mshirika ambaye hakufanikiwa kumkumbuka jina mara moja ambaye
amefariki akiwa hospitalini.
Aidha akiongea kwa masikitiko askofu
wa jimbo la Tabora Mhashamu Issaya Ilumba amewataka madreva kuwa waangalifu
wanapokuwa wanawaendesha viongozi mbalimbali na si kanisa hilo bali Taifa zima
kuwa waangalifu kuepusha ajali.
Ajali hiyo imetokea majira ya saa
tisa na nusu 21/04/2016, baada ya gurudumu la mbele kushoto, la gari aina ya Toyota
Prado lenye namba za usajili TNA kupinduka mara mbili na kusababisha vifo
viwili papo hapo na mmoja katika hospitali ya rufaa ya Kitete Tabora.
Post a Comment