Header Ads

MASHINE ZA CT SCAN NA MRI ZAANZA KUFANYA KAZI.


Baada ya agizo la Rais John Magufuli kutembelea hospitali ya Taifa Muhimbili..aliagiza badhi ya mambo kufanyiwa utekelezaji ikiwemo mashine za CT Scan na MRI ambazo zilikuwa na matatizo kutengenezwa ili kuwasaidia wagonjwa.

Leo Katibu mkuu wa Wizara ya Afya Donan Mbando ametembelea hospitali hiyo na kukagua maeneo mbalimbali na kuzindua duka la dawa la MSD pamoja na kukagua mashine za CT Scan na MRI ambazo kwa sasa tayari zimeanza kufanya kazi kama kawaida.

Mengine kutoka katika taarifa yake Mbando amesema kumekuwa na changamoto ya kuwapeleka wagonjwa wengi nje ya nchi ikiwemo wa moyo, figo na saratani lakini kama Serikali wamejitahidi kuhakikisha wanajenga uwezo wa kuhakikisha huduma hizo zinapatikana ndani ya nchi.

Wagonjwa wanaokwenda nje ya nchi sasa kutibiwa ndani ya nchi...“Hawa wagonjwa tungewapeleka nje tungetumia zaidi ya milioni 500, mwaka huu tumetenga bajeti bilioni 5 ya kuwaleta wataalam kuja kufanya kazi hapa ili kupunguza gharama ya kusafirisha wagonjwa, mfano sasa hivi ukitembelea India kwa sasa wagonjwa wengi ambao walikuwa wakipelekwa huko wamepungua sana, na itafika wakati kutakuwa hakuna kabisa wagonjwa kwenda kutibiwa nje”Donan Mbando.

Watalamu wa mafunzo kutoka Marekani tayari wamewasili nchini..”Kuna wataalamu kutoka Serikali ya Marekani ambao tayari wamewasili na kutoa mafunzo itasaidia kupunguza gharama kupeleka wagonjwa nje ya nchi, tungewapeleka nje ya nchi tungetumia milioni 500, tulitenga bajeti bilioni 5 bajeti ya mwaka huu kwa kuleta wataalam kuja kufanya kazi hapa, naamini tunapojenga uwezo kwa wataalam wa hapa nyumbani itasaidia kupunguza gharama..

Kuhusu deni la mashine za MRI na CT Scan Mbando aliongeza kuwa… “Haiingii akili ninakupa kifaa kinakuingizia mapato bado unataka Serikali itoe fedha za matengenezo, tumetoa amelekezo kuwa baadhi ya mapato yatengwe kwa ajili ya kutengeneza vifaa tiba.

"Kila hospitali za Mikoa na kanda zitenge bajeti ya kutengeneza vifaa vyao, mfano una mashine inayokutengenezea kiasi cha milioni 100 kwa mwezi bado unataka mtu mwingine atoe pesa yake kukutengenezea kifaa hicho, siyo sahihi?…Serikali imenunua vifaa tiba kwa ajili ya kutoa huduma kwa hospitali zote nchini.

Kuhusu deni la MSD Mbando alisema..."Tunatakiwa kama Serikali kuchangia bilioni 10, tumelipa milioni 42 na tumeweka programu maalumu ya mapokezi ya dawa kwamba kila anayetaka kutusaidia msaada wa dawa ziwe hazijapungua matumizi kuanzia miezi sita na kuendelea, deni lililobaki tutaendelea kulilipa kwa utaratibu, jumla ya deni tunalodaiwa ni zaidi ya bilioni 120 lakini lililohakikiwa na mkaguzi mkuu wa Serikali ni bilioni 53 na tutaliingiza kwenye bajeti yetu”Mbando.

Taarifa ya mashine za CT Scan na MRI kuanza kufanya kazi.Mkuu wa Idara ya Radiologia Flora Lwakatare amesema.. “Tumeanza kutumia mashine hizo baada ya kufanyika matengenezo na tayari jumla ya wagonjwa 76 wametumia mashine ya MRI huku wagonjwa 152 wakiwa wameshatumia mashine za CT Scan”..Lwakatare

No comments