Header Ads

TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA YALAANI VITENDO VYA KIKATILI DHIDI YA WATU WENYE UALBINO.


Tume ya haki za binadamu na utawala bora imelaani juu ya vitendo vya kikatili vilivyoibuka tena hivi karibuni katika baadhi ya mikoa vya kufukua makaburi ya watu wenye ualbino kunakotokana na imani za kishirikina na kuitaka serikali kuongeza juhudi zaidi katika kupambana na watu wanaofanya uhalifu huo.
Mwenyekiti wa tume hiyo Bw.Bahame Tom Nyanduga amesema hayo jijini Dar es Salaam mara baada ya kikao kilichohusisha wadau mbalimbali kutoka taasisi mbalimbali kukemea vitendo hivyo vya kikatili na kusema kuwa bado juhudi zaidi zinahitajika katika mapambano hayo ili kukomesha kabisa vitendo hivyo.
Bw.Nyanduga pia amezitaja changamoto mbalimbali zinazorudisha nyuma juhudi mbalimbali za serikali na vyombo vyake katika kupambana na vitendo hivyo ikiwemo mkanganyiko wa takwimu juu watu wenye ualbino waliopotea ambavyo vinakwamisha ushughulikiaji wa wahalifu huku ofisi ya mwendesha mashtaka mkuu (DPP) ikitaja kesi ambazo zimeshashughulikiwa mpaka sasa.

No comments