Header Ads

Fahamu Kuhusu Misukule Wa Maofisini Na Jinsi Ya Kujikinga Usifanywe Msukule Wa Ofisini


Na. Dokta  Mungwa  Kabili...0744  000 473

SWALI : Mtaalamu, kwa  heshima  na  taadhima  ninaomba  unisaidie  suala  langu. Mimi ni  mwanamke  mkaazi  wa  manispaa  ya  Nyamagana, jijini  Mwanza,  umri  wangu ni  miaka  37, mume  wangu ana  miaka  45 sasa.  Tangu  tumefunga  ndoa, huu  ni  mwaka  wa  kumi na  tano.  Mimi   nina jishughulisha  na  biashara  ya  ufundi cherehani. Mume  wangu amesoma hadi  Chuo  Kikuu, amesomea  mambo ya  kompyuta.
 
Tangu mwaka  2000  mume wangu  amekuwa  akifanya  kazi  kwenye  Internet  Café ya  Muhindi . Hela  anayo  lipwa kidogo sana, na  kutokana  na  uchapaji  kazi  wake, kampuni  nyingi zimekuwa  zikimfuata  zikitaka  kumuajiri tena  kwa  kulipa  hela  nyingi  zaidi  ya zile  anazo lipwa  kwa  huyo tajiri muhindi.
Unyayo

Lakini  cha  kushangaza mume  wangu  amekuwa  akiwakatalia. Maisha  tunayo  ishi hayaridhishi hata kidogo, tunazidiwa  mpaka  na  vijana  wadogo  walio anza  maisha  juzi tu. Nikimwambia  mume  wangu, atafute  sehemu  yenye  maslahi, anakataa. Nikiwambia  tutunze  hela, afungue  nay eye  internet  café yake, anakataa  pia, yeye  amekazana  na  kumtumikia  huyo  muhindi.

Siku moja  nikiwa  naongea  na  shoga  yangu  mmoja, akaniambia  inawezekana  mume  wangu  atakuwa  amefanywa  msukule  wa  ofisini  na  huyo  bosi  wake  muhindi.  Eti  mtaalamu, hivi  ni  kweli, jambo  hilo  linawezekana kwamba  kweli  mume  wangu  amefanywa  msukule  wa  kazi  na  bosi  wake ?  kama  ni  kweli ninamtoaje  kwenye  huo  utumwa ?

DR. MUNGWA  KABILI  ANAJIBU.
Pole  sana  dada  angu  kwa  madhila  yaliyo mkuta  mume  wako.   Ni kweli  kabisa, wapo misukule  wa  ofisini.  Uchawi  huu, hufanywa  na  wamiliki  wa  kampuni  na  biashara  mbalimbali. Walengwa  wakuu  wa  uchawi  huu  ni  kwanza wafanyakazi  wachapakazi   walio  na  weledi  wa  kazi  husika, na  pili wafanyakazi  ambao  nyota  zao  zinaendana  na  biashara  husika.

Wapo  misukule  wa  aina  mbili. Misukule  wanao  onekana  kwa  macho  ya  nyama, na  misukule wasio  onekana.
 
Misukule wasio  onekana  ni watu  wanao  dhaniwa  kufa, lakini  kiukweli  wanakuwa  hawajafa, isipokuwa  wanakuwa  wamechukuliwa  kichawi.
 
Ilihali  misukule  wanao  onekana, ni  watu  wanaoishi  kama  watu  wengine, lakini  nyota  zao zinakuwa  zimechukuliwa  na  wachawi  kwa matumizi  yao  binafsi (wachawi ) na  pia  nafsi.

KUFAHAMU  KWA  UNDANI  KUHUSU  MISUKULE  WASIO  ONEKANA, TAFADHALI TEMBELEA :

Misukule wa  maofisini  wapo  katika  kundi  la  misukule  wanao  onekana .  Watu  hawa hupumbazwa kufungwa  kichawi  na  kufanywa  watumishi  wa  walio  wapumbaza, kwa  kadri  walivyo  nuiziwa.  Wapo  walio nuiziwa  kuwatumikia  mabosi  wao kwa  miaka kumi, wengine  ishirini, wengine  thelathini  na w engine  katika  maisha  yao  yote.
 
Msukule  huyu  anaweza  kuwa  bar maid, meneja  wa  bar, House  Girl, House  Boy, Mkata  majani, mkurugenzi  wa  kampuni kubwa, Mwalimu, daktari,mwanasheria, fundi wa  magari, Mtayarishaji  wa  muziki, muuza  mayai, au  Ice  Cream  nakadhalika.

JINSI  MISUKULE  WA MAOFISINI  WANAVYO  TENGENEZWA.
Ili kumtengeneza mtu na  kumfanya  awe msukule  wa  ofisi mambo  yafuatayo  hufanyika.
 
Kwanza  zinachukuliwa  nyayo  zake, kisha  zinafungwa  kwenye  kitambaa  cheusi  pamoja  mchanganyiko wa  miti  ya  kichawi ya  aina  arobaini  na  dua  maalumu  ya  kumfunga  muhusika.

Pili  linachimbwa  shimo lenye  urefu  wa  futi  saba, ndani ya  shimo hilo inafanyika  kafara  ya PUNDA  MWENYE  ALAMA  YA  MSALABA  MGONGONI  na  kondoo  mwenye  rangi  nyeusi  bila  doa  lolote, halafu nyayo  za  mtu   huyo  zilizo  fungwa  kwenye  kitambaa  cheusi zikiwa pamoja  na  miti  arobaini  ya  kichawi na  dua  yake, vinatupiwa  kwenye  shimo  hilo  huku  maneno  Fulani  ya  kichawi  yakitamkwa.

Baada  ya  hapo  litachukuliwa jiwe  lenye uzito  unao endana  na  idadi  ya  miaka  ambayo  mchawi  anataka  kumtumikisha  muhusika.

Kama  anamtaka  kwa  mwaka mmoja, basi  jiwe  huwa  na  uzito  wa  kilo  moja, kama  ni  miaka  kumi  basi  jiwe  huwa  na  uzito  wa  kilo  kumi, kama  ni  miaka  thelathini, basi  mawe  yawe  na  uzito  wa  kilo  thelathini, na  kama  anataka  kumtumikisha  maisha  basi  ataweka mawe  yenye  uzito wa  kilo  hamsini hadi  miaka. Mawe  hayo  hukandamiza hicho  kitambaa.

Baada  ya  hapo shimo  hilo  litafukiwa  kwa  udongo  wa makaburini. Mambo  haya  yakisha fanyika, utachukuliwa  mchanga wa  kwenye  kivuli cha muhusika, utachanganywa  na  dawa nyingine  za  kichawi  ambazo idadi  yake  ni  tisa, vitu vitafungwa  kwenye  kitambaa  cheusi, na  kuhifadhiwa  kwenye  kibuyu  au  chungu cheusi  chenye  dawa  za  kichawi  kwa  siku  saba, baada  ya  hapo  atachukuliwa  kuku  mweusi  ambaye  ataunguzwa  kwenye  chungu  cheusi  akiwa  mzima  hadi  awe majivu.

Majivu  hayo, yatagawanywa mara  mbili, kisha  fungu la kwanza  atalishwa  PUNDA  MWENYE  ALAMA  YA  MSALABA  MGONGONI  na  kisha  atazikwa  akiwa mzima  mzima, na  fungu  la  pili  atalishwa  kondoo  mweusi   na  kuzikwa  akiwa  mzima  mzima.

Baada  ya  hapo  litafanyika  tambiko  jingine  la kafara  ya  PUNDA  MWENYE  ALAMA  YA  MSALABA  MGONGONI  na  kondoo mweusi.

Kabla  ya  kuchinjwa  kondoo  pamoja  na  punda  hao  watalishwa  dawa  fulani  za  kichawi, na  baada  ya  kuchinjwa nyama  ya  punda  na  kondoo  watakao  tolewa  kafara, itatumika  kumlisha  mtu  au  watu  walio  kusudiwa. Mara  nyingi  huwa  kwenye sherehe, hafla, au  anaweza  kukuita  nyumbani  kwake, kisha  nyama  husika  ikawa  kitoweo chako.
 
MTU  AKIFANYIWA  ULOZI  HUU, HUWA  MTUMISHI  MTIIFU   KATIKA  MAISHA  YAKE  YOTE.  AINA  HII  YA  ULOZI  HUTUMIKA  PIA  KATIKA  MAPENZI.

Jinsi  Ya  Kujikinga  Na  Ulozi  Huu:
Ili  kujikinga  na  ulozi  huu, mhusika  afanyiwe  tambiko  maalumu  la  kumkinga  dhidi  ya  uchawi  na  ulozi  wa  aina  yote  ile. Na  kama  tayari  mtu ameshafanyiwa  ulozi  huu, basi  lifanyike  tambiko  maalumu  la  kurudisha  nyota  yake  na  kumfungua  kutoka  kwenye  kifungo  hicho.
 
Katika  tambiko  hilo, ni lazima  sehemu  iliyo  tumika  kuzika  unyayo wa  muhusika, igunduliwe na  kisha  tambiko  maalumu  likafanyike  katika  eneo  hilo.

KWA   MAKALA  KUHUSU  ULIMWENGU  USIO ONEKANA, TEMBELEA  KILA  SIKU:

No comments