Zimbabwe yazindua fedha zake kwa mara ya kwanza
Noti mpya za Zimbabwe.
Taifa la Zimbabwe limezindua fedha zake kwa mara ya kwanza tangu sarafu ya dola ya taifa hilo ifutiliwe mbali miaka saba iliyopita kufuatia mfumuko mkubwa wa kiuchumi.
Noti hizo ambazo zilizinduliwa kwa mara ya kwanza mnamo mwezi Mei, zimesababisha maandamano makubwa katika kipindi cha muongo mmoja dhidi ya rais Mugabe .
Serikali imesisitiza kuwa noti hizo za dhamana siyo sarafu rasmi ya taifa hilo imezindua noti hizo ili kukabiliana na upungufu wa fedha na kusitisha matumizi ya dola ya Marekani ambayo inazidi kutolewa nje ya taifa hilo, hatua ambayo kundi la wafanyibiashara wameiunga mkono.

Post a Comment