Header Ads

Wakazi wa wilaya ya Ukerewe, wanalazimika kula mlo mmoja kutokana na upungufu wa chakula, uliosababishwa na hali ya ukame.



Baadhi ya wakazi wa wilaya ya Ukerewe, wanalazimika kula mlo mmoja kwa siku kutokana na kukabiliwa na upungufu wa chakula, uliosababishwa na hali ya ukame pamoja na zao la muhogo ambalo ni tegemeo kubwa la chakula kwa wananchi wa wilaya hiyo kuugua ugonjwa wa Batobato kali.Hali hiyo imebainishwa na mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Ukerewe Gorge Nyamaha.

Diwani wa kata ya Bukanda Willibart Mbando ameiomba ofisi ya mkuu wa wilaya ya Ukerewe kupitia kamati ya maafa kutoa vibali kwa wafanyabiashara vya kuagiza chakula cha msaada pamoja na cha bei nafuu ili kusaidia kupunguza makali ya njaa, huku diwani wa kata ya Muriti Makole Chilato akisema upungufu huo wa chakula katika baadhi ya kaya umechangia kushuka kwa mahudhurio ya wanafunzi mashuleni.

Samson Ibrahim ni mkuu wa idara ya kilimo, umwagiliaji na ushirika wilayani Ukerewe anasema kulingana na hali ya mavuno msimu uliopita, ilitarajiwa kuwa wilaya hiyo ingekuwa na ziada ya tani 2,735 hadi kufikia mwezi Aprili mwakani badala yake hali ya ukame wa muda mrefu imesababisha chakula hicho kutofikia muda huo.

No comments