Maelfu waandamana kumpinga rais wa Korea Kusini
Maandamano mjini Seoul
Mandamano ya leo yanatarajiwa kuwa makubwa zaidi. Viongozi wa maandamano hayo wanasema mamilioni ya watu watashiriki.
Maelfu ya maafisa wa polisi wa kukabiliana na ghasia,wamepelekwa katika mji mkuu wa Seoul kukabiliana na waandamanaji hao wanaopinga serikali kufika ikulu ya rais.
Rais Park Guen Hye
Rais Park Guen Hye, anatuhumiwa kwa kuwa na uhusiano wa karibu na Choi Soon-sil, anayekabiliwa na shtaka la kujaribu kuibia serikali fedha nyingi kupitia kampuni kadhaa za taifa hilo.
Maafisa kadhaa wanaohudumu katika ofisi ya Rais Guen Hye pia wanachunguzwa dhidi ya sakata hiyo.


Post a Comment