Header Ads

VIDEO: Rais Magufuli awapa Siku 15 Wakuuu Wa Mikoa Kuondoa Majina ya Wafanyakazi Hewa Wanaolipwa Mishahara....Tazama Video hii

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli amesema jumla ya wafanyakazi 202 katika halmashauri 14 katika mikoa ya Singida na Dodoma waligundulika kuwa hewa na kulipwa mishahara kila mwezi.

Rais ameyasema hayo alipokuwa akiwakumbusha wakuu wa kikoa wapya ambao amewaapisha leo Ikulu jijini Dar es salaam.

''Kwa mikoa miwili tuu wafanyakazi hao 202 wanalipwa mishahara hewa na kwenye data ilionyesha wengine wamefariki, wamestaafu, wamefukuzwa , wengine likizo bila malipo wote hao kumbe wanalipwa malipo ya serikali fedha ambazo zingetumika kutatua matatizo ya wananchi''.Amesema Rais Magufuli

Kwa msingi huo kwa halmashauri 180 nchini ina maana kwa mahesabu ya haraka haraka kuna wafanyakazi 2000 na zaidi wanalipwa mishahara hewa.

Hivyo Rais Dkt Magufuli ametoa agizo kwa wakurugenzi wa taasisi za serikali kuanzia leo ndani ya siku 15 kuhakikisha wanapitia majina ya waajiriwa wote wa serikali na kuondoa majina ya ambao wanalipwa bila kufanya kazi.

==>Tazama Video hii Kumsikiliza Rais Magufuli Akiongea


No comments