Header Ads

CCM NYAMAGANA KUMSAFIRISHA KWA NDEGE MSANII ALIETEMBEA KWA MIGUU KUTOKA JIJINI MWANZA HADI DAR.




Rafael Shilatu ambae ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Nyamagana (Kulia) akizungumza katika hafla ya kumpongeza msanii Rich4D.
Na:George Binagi-GB Pazzo @BMG.
Chama cha Mapinduzi CCM kimekubali kumsafirisha kwa ndege Mwanamuziki Chipukizi Richard Stanford maarufu kwa jina la Rich4D, alietembea kwa miguu kutoka Jijini Mwanza hadi Jijini Dar es Salaam ili kumpongeza Rais Dkt.John Pombe Magufuli kwa kuwajumuisha Wasanii katika Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.

Mwenyekiti wa Chama hicho Wilaya ya Nyamagana Mkoani Mwanza Raphael Shilatu, alitoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki iliyopita, katika hafla ya kumpongeza msanii huyo kwa matembezi yake baada ya kurejea Jijini Mwanza.

"Kwanza nimpongeze kwa matembezi yake ambayo ni ya kizalendo kabisa. Lakini niseme kwamba atakapopata fursa ya kwenda kuonana na Mhe.Rais, tutamsafirisha kwa ndege kutoka Jijini Mwanza hadi Jijini Dar na kumrudisha pia". Alisema Shilatu huku akimuomba Katibu Mkuu Mhandisi John Kijazi kumsaidia msanii huo ili aweze kuonana na Mhe.Rais Dkt.Magufuli.

Januari 16 mwaka huu Msanii Rich4D alianza matembezi yake kutoka Jijini Mwanza na kupita katika Mikoa Minane sawa na kilomita 1,200 hadi kufika Jijini Dar Februari 10, hii ikiwa ni siku 26 mfululizo za matembezi hayo ambayo mbali na kumpongeza Rais Dkt.Magufuli, pia yalilenga kuwasilisha kilio cha wasanii chipukizi wa Mikoani ambao wamekuwa wakikosa fursa mbalimbali ikilinganishwa na wasanii wakubwa walioko Jijini Dar.

"Kila Mkoa na Wilaya nilizopita nilipokelewa na viongozi mbalimbali wakiwemo Maafisa Utamaduni na baada ya kufika Dar nilipokelewa na Viongozi wa Serikali akiwemo aliekuwa Katibu Mkuu Ombeni Sefue ambae aliniahidi kuonana na Mhe.Rais kabla mwezi wa pili haujaisha kwani nilishindwa kuonana na rais baada ya kuambiwa yuko katika majukumu mengine ya Kitaifa". Alitanabaisha Rich4D na kumuomba Katibu Mkuu mpya Mhandisi John Kijazi kuhakikisha ahadi aliyoiacha Sefue inatimia.
Msanii Rich4D akionyesha Vibali alivyokuwa navyo kabla ya kuanza matembezi yake.

Msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya kutoka Jijini Mwanza, Joseph Stanford, maarufu kwa jina la Rich4D akiwaonyesha wanahabari Jijini Mwanza (hawapo pichani) ramani ya Mkoa wa Dar es salaam aliyoitumia kutambua maeneo ya Mkoani huo.



Msanii Rich4D akizungumzia matembezi yake ya Miguu kutoka Jijini Mwanza hadi Jijini Dar. Kutoka Kushoto waliokaa ni Gaspar Babu ambae ni Meneja wa Klabu ya Fussion Jijini Mwanza ambae pia alikuwa Mratibu Msaidizi wa Matembezi ya Rich4D, Jamal Abdul ambae ni MNEC Mkoani Mwanza, Raphael Shilatu ambae ni Mwenyekiti wa CCM Wilayani Nyamagana, Mbunge wa Jimbo la Nyamagana (CCM) Stanslaus Mabula, Alphonce Tonny Kapela ambae ni Mratibu wa Matembezi hayo.


Alphonce Tonny Kapela ambae ni Mratibu wa Matembezi hayo akizungumzia matembezi ya Msanii Rich4D ambapo amempongeza msanii huyo kwa matembezi hayo ya kizalendo.

Kutoka Kushoto waliokaa ni Gaspar Babu ambae ni Meneja wa Klabu ya Fussion Jijini Mwanza ambae pia alikuwa Mratibu Msaidizi wa Matembezi ya Msanii Rich4D, Msanii Rich4D, Jamal Abdul ambae ni MNEC Mkoani Mwanza, Raphael Shilatu ambae ni Mwenyekiti wa CCM Wilayani Nyamagana, Mbunge wa Jimbo la Nyamagana (CCM) Stanslaus Mabula


Mbunge wa Jimbo la Nyamagana (CCM) Stanslaus Mabula (kulia) amepongeza matembezi ya Msanii Rich4D ambayo ni ya kizalendo na yanayofaa kuigwa na vijana wengine. 




Mabula alijitoa kwa hali na Mali katika kusaidia Matembezi ya Msanii Rich4D baada ya kubaini mapungufu aliyokuwa nayo ikiwemo kutokuwa na pesa kwa ajili ya chakula na marazi na ameahidi kuendelea kuyasaidia makundi mbalimbali katika jamii yanayoonyesha nia na uzalendo kama wa msanii Rich4D.


Picha ya Pamoja ambapo kutoka Kushoto ni Gaspar Babu ambae ni Meneja wa Klabu ya Fussion Jijini Mwanza ambae pia alikuwa Mratibu Msaidizi wa Matembezi ya Msanii Rich4D, Jamal Abdul ambae ni MNEC Mkoani Mwanza, Msanii Rich4D, Mgeni rasmi Raphael Shilatu ambae ni Mwenyekiti wa CCM Wilayani Nyamagana, Mbunge wa Jimbo la Nyamagana (CCM) Stanslaus Mabula na Alphonce Tonny Kapela ambae ni Mratibu wa Matembezi hayo ya Msanii Rich4D.





No comments