Header Ads

HALMASHAURI YA WILAYA GEITA YATUHUMIWA KWA WIZI.



Chama cha mapinduzi ccm,mkoani Geita,kimemtaka mkurugenzi wa wilaya ya Geita,kuchunguza na kuunda tume ya kufatilia ufisadi wa kiasi cha sh,milioni 300 kati ya sh,billion 1.2  zilizotolewa kwa ajili ya ununuzi wa mitambo ya ujenzi wa barabara.

Kauli hiyo imetolewa na mwenyekiti wa ccm mkoani hapa,na mbunge wa jimbo la Geita,Joseph Kasheku Msukuma,wakati wa kikao cha kwanza cha baraza la madiwani kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya ya geita.

Amemtaka mkurugenzi kutokukubali kupokea mitambo  bila ya kuwa na taarifa kamili ya vitu ambavyo vimepungua katika mitambo hiyo.
Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya hiyo,Elisha Lupuga, amekili kusaini mikataba  ya kupokea mitambo hiyo bila ya kujua kuwa mitambo hiyo ilikuwa chini ya kiwango.
Aidha mkurugenzi wa halmshauri ya wilaya,Ally Kidwaka,amesema kuwa mitambo hiyo bado haijapokelewa na kwamba ameunda tume ya  watu wanne kuhakikisha wanafuatilia na kuchunguza ubora  wa mitambo hiyo.


Mkuu wa wilaya ya geita,Manzie Omary Manguchie,amewataka madiwani hao kufanya kazi kwa uadilifu na uaminifu na kuachana na vitendo vya rushwa ambavyo vimekuwa vikisababisha kushuka kwa maendeleo katika wilaya hiyo.

No comments