Header Ads

RAIS MAGUFULI HONGERA TUNAAMINI HIZI CHANGAMOTO UZITAZITATUA.

                                                            MGUSU                      


Ni kijiji kilicho upande wa magharibi mwa mji wa Geita takribani kilometa 25 kutoka Geita mjini.

Kilianza mnamo Novemba 1987,shughuli kuu za kiuchumi katika kijiji hicho ni uchimbaji wa madini.Mpaka sasa kijiji hiki kina zaidi ya watu 12,000 ambapo tayari kimepewa hadhi ya kuwa kata kutokana na wingi wa watu.Kijiji hiki ni moja kati ya vijiji vyenye changamoto nyingi ikiwa ni pamoja na ukosefu wa miundo mbinu muhimu kama barabara,afya,maji na Elimu.                                                                                                                     AFYAMpaka sasa kijiji hiki hakina zahanati wala kituo cha afya hali inayopelekea baadhi ya vifo vya kina mama wakati wa kujifungua kutokana na umbali wa huduma hiyo muhimu ya afya ambapo watu hulazimika kusafiri umbali mrefu hadi Geita mjini kuifuata.
                                             ELIMUKatika kijiji hiki pia kuna shule moja ya msingi ambayo ina zaidi ya watoto 1000,hata hivyo shule hii inakabiriwa na changamoto lukuki ikiwa ni pamoja na ukosefu wa madawati,madarasa machache ambapo ndani ya chumba kimoja cha darasa hulazimika kukaa watoto zaidi ya mia moja,changamoto nyingine ni pamoja na walimu wachache,vitabu na zana nyingine za kufundishia.
Hali hii inawafanya walimu walio katika shule hii kuwa na wakati mgumu sana katika kutekeleza majukumu yao na kufanya kiwango cha elimu kuwa duni shuleni hapo.
Upande wa shule ya sekondari nayo pia ipo moja(SHANTAMINE) ambayo ni ya kata nayo hata hivyo ipo umbali wa zaidi ya kilometa 18 kutoka kijijini hapo.Wanafunzi wanaosoma katika shule hii wanakabiriwa na wakati mgumu kwani wengi wao huwawia vigumu kufika shuleni hapo kutokana na umbali uliopo ambapo nauli kufika shuleni kwenda na kurudi ni shilingi 5000,wengi wao wanatoka familia maskini ambapo wakati mwingine huomba msaada(lift) kwenye malori ili kufika shuleni.
Hata hivyo si wote wanaoanza kidato cha kwanza hufanikiwa kuhitimu masomo yao hasa watoto wa kike kwani wengi huishia kubeba ujauzito na kujikuta ndoto zao kuishia njiani.



Mambo mengine yanayokikabili kijiji hicho ni pamoja maji kutokuwa safi kwani maji wanayotumia kwa kiasi kikubwa yamezungukwa na maeneo ya uchanjuaji wa dhahabu kwa kutumia madini ya mecury( zebaki) ambayo ni hatari kwa afya ya binadamu.
Mjumbe wa Serikali ya kijiji Bwana John Peter anasema wao kama serikali ya kijiji wafanya jitihada za kuongea na uongozi wa Wilaya ili kutatua changamoto hizo ambapo hata hivyo hakuna utekelezaji wowote mbali na ahadi.Anaiomba serikali ikitazame kwa jicho la tatu kijiji hicho kilichozungukwa na madini lakini hali yake bado ni mbaya sana.



IMEANDALIWA NA: Paul William (Geita)

No comments