Header Ads

WIZKID ATENGULIWA UBALOZI MTN.

Lagos, Nigeria
MKALI wa AfroPop kutoka nchini Nigeria, Ayodeji Balogun ‘Wizkid’ametenguliwa kuendelea kuwa Balozi wa Kampuni la MTN kama alivyokuwa hapo mwanzo.
Kwa mujibu wa vyanzo vya karibu kutoka kampuni hiyo inayohusika na mawasiliano, inadaiwa kuwa Wizkid amesitishwa kuendelea kuwa balozi baada ya kuonekana kuwa hana faida, wakati msanii Wizkid akitenguliwa ubalozi wenzake Davido, Don Jazzy,Tiwa Savage na Iyanya wakipewa mikataba mipya.
“Kuna wasanii wengi sana wanaofanya vizuri nchini Nigeria tunawaomba waendelee kuweka kazi zao katika mitandao ya muziki muda ukifika tukiwahitaji tutawachukua,” alisema Iweanoge, msemaji wa MTN.GP

No comments