UANDIKISHAJI BVR,KOMPYUTA YAIBIWA GEITA.
Kompyuta ya kutunzia kumbukumbu za watu waliojiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura wilayani Nyang'hwale imeibiwa na watu wasiojulikana katika kijiji cha Mabongo,kata ya Nyugwa mkoani Geita.
Mkuu wa Wilaya ya Nyang'hwale Ibrahim Marwa amethibitisha kuibiwa kwa kompyuta hiyo na kusema imetoweka katika mazingira ya kutatanisha.
Hata hivyo alisema polisi wilayani humo inawashikilian watu watano,akiwemo mwandikishaji mkuu na msaidizi wake.
Marwa alisema tukio hilo lilitokea jumamosi iliyopita asubuhi wakati wakihamisha vifaa hivyo kutoka kwenye moja ya kituo katika kata hiyo kwa ajili ya kuendelea na kazi ya uandikishaji.
Alisema wakati waandikishaji wanaanza kupanga mashine zao,ndipo walibaini kutokuwapo kwa mashine hiyo.
Post a Comment