Header Ads

SALOON ILIYOKO SINZA..INAYOFANYA MASAJI HUKU IKIJIHUSISHA NA UTOAJI WA HUDUMA YA NGONO CHAFU

AMA kweli shetani anafanya hesabu zake za mwisho! Tangu mwaka  uanze yapo yaliyotokea na kusisimua likiwemo la kunaswa kwa kinara wa utoaji mimba, Dar lakini hili la warembo kufumwa wakitoa dozi ya ngono linaweka historia nyingine,

Warembo wanaotoa huduma wakiwa wameficha sura zao baada ya kunaswa na OFM.

Hebu sikia, saluni inayojihusisha na vitendo vya ’masaji’ lakini kumbe ngono imo ndani yake imenaswa na kufumuliwa baada ya kukutwa uchafu wa aina yake nyuma ya pazia.

Saluni hiyo maarufu kuliko Miji ya Sodoma na Gomora, ipo maeneo ya Sinza ambapo kwa muda mrefu sasa imekuwa ikijihusisha na uchafu huo na kusababisha kero kwa wananchi wenye maadili yaliyotukuka.

No comments