Header Ads

BENDERA YA KIKOLONI KUONDOLEWA S.CAROLINA.

Bendera ya kikoloni kuondolewa kwenye makao makuu ya mji wa South Carolina Marekani
Maseneta wa jimbo la South Carolina nchini Marekani wamepitisha sheria inayoharamisha kupeperushwa benderea ya kikaburu iliyotumika nchini humo wakati wa utumwa.
Hatua hii inafuatia kisa cha mwanamume aliyewapiga risasi na kuwaua waumini wa kikristu weusi katika kanisa moja mwezi Juni.
Mwanamume huyo Dylann Roof 21, alionekana katika baadhi ya picha zake akipeperusha bendera hiyo.
null
Kampeini ya kuondolewa kwa bendera hiyo ilianza baada ya mauaji ya watu 9 weusi mwezi juni
Kwa miaka mingi bendera hiyo imechukuliwa kuwa ishara ya ubaguzi wa rangi na udunishwaji wa watu wa rangi nyeusi na vizazi vyao.
Sasa sheria hiyo inasubiriwa kuidhinishwa na bunge la waakilishi.
Hata hivyo sharti itekeleze sharti la kupigiwa kura na thuluthi mbili ya wabunge kabla haijatiwa sahihi na kuidhinishwa na gavana kuwa sheria.
null
Dylann Roof aliyewapiga risasi na kuwaua waumini wa kikristu weusi katika kanisa la Charlstone mwezi Juni.
Wajumbe kadhaa walioipigia kura kauli hiyo walisema kuwa walivutiwa na msamaha uliodhihirika kutoka kwa jamaa ya waliofiwa baada ya shambulizi hilo lililovutia hisia nyingi.
Roof aliishambulia kanisa la kihistoria la Emanuel AME juni 17 na kuwaua watu 9 akikusudia kuanzisha uhasama baina ya wazungu na watu weusi.BBC

No comments