Header Ads

Ethiopia imezima mitandao ya kijamii



Mitandao ya kijamii nchini Ethiopia imezimwa.
Waethiopia waliamka Wikiendi wakajipata hawana huduma hizo za mitandao kama Facebook, Twitter, Instagram na Viber.
Serikali imefunga mitandao hiyo tangu Jumamosi usiku.
Msemaji wa serikali ameiambia shirika la habari la AFP kuwa serikali ilichukua hatua hiyo kama njia ya kuzuia wanafunzi wasivurugwe na ushawishiwa mitandao hiyo ya kijamii.
Hatua hiyo vilevile imetokea majuma kadhaa baada ya baadhi ya makaratasi ya mitihani kuchapishwa kwenye mitandao ya kijamii na kulazimu serikali kufutilia mbali mitihani hiyo iliyodukuliwa.
''Serikali imechukua hatua hiyo kwa muda hadi siku ya Jumatano.
Tumegundua kuwa mitandao ya kijamii huvuruga kabisa ratiba ya vijana na haswa wanafunzi'', alisema msemaji wa serikali Getachew Reda .
Hatu hiyo bila shaka imewaudhi wanaharakati wa kupigania uhuru wa habari nchini Ethiopia.
Mwanabloggu mashuhuri Daniel Berhane amechapisha kwenye mtandao wake wa Twitter maswali ambayo anataka yajibiwe.
Je ni nani aliyechukua uamuzi huu?
Aliwashauri kina nani ?
kwanini alichukua hatua hiyo?
Je hii haitakuwa mwanzo wa tatizo lipya la kukandamiza uhuru wa kujieleza ?
CHANZO:BBC

No comments