Header Ads

WAKULIMA MKOANI GEITA WAHAMASIKA KULIMA KISASA NA KAMPUNI YA AGRICS.

Hata hivyo kampuni hiyo imeendelea kuwasisitiza wakulima ambao hawajajisajili katika mradi kufanya hivyo mapema kwani wakati unayoyoma. 

Fursa hii ya mkopo wa mbegu za mahindi, alizeti, mbolea ya kisasa, na sola kwa ajili ya mwanga kwa mkopo nafuu kabisa inalenga kuwainua wakulima na kuwafanya wahame katika kilimo cha mazoea na kufanya kilimo biashara.
Akiongea kwa niaba ya kampuni hiyo Mratibu wa kampuni mkoa wa Geita Bwana Semeni Kime amewashukuru wananchi kwa kuchangamkia fursa hiyo na pia amewataka waendeleee kujiunga kwa wingi kwani hii ni fursa ya kipekee kwa maendeleo ya mkulima.

Pia amewatoa hofu wakulima wa Geita juu soko la zao la alizeti kwani Agrics itashirikiana na kampuni dada iitwayo Alizetics kununua alizeti ili kuwakikishishia soko la zao hilo.

Usajili utafika tamati mwezi wa sita mwishoni hivyo wakulima wanaombwa kuchukua hatua za maksudi kuhakikisha maendeleo ya mkulima na Geita kwa ujumla yanasonga mbele.
Semen Kime-Mratibu wa kampuni (Agrics) mkoa wa Geita

No comments