SERIKALI KUDHIBITI TATIZO LA MILIPUKO YA MGODINI GEITA.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani, (wa kwanza kushoto), akiongozwa na Meneja Mwandamizi Miradi ya Umeme wa TANESCO pamoja na wafuasi wengine.
Mbunge wa geita mjini Mh Costantine Kanyasu
Wananchi wa kata ya mtakuja mtaa wa Nyamalembo, Katoma na Kompaund wilayani Geita, wamefikisha malalamiko yao kwa Naibu Waziri wa nishati na madini,mh Dr.Medadi Kalemani juu ya nyumba zao kuendelea kubomoka kutokana na upasuaji wa miamba unaofanywa na kampuni ya uchimbaji wa madini GGM mkoani Geita.
Wakizungumza katika ofisi za serikali ya mtaa wamesema kuwa ni vyema kwa naibu waziri kuangalia uwezekano wa kuhakikisha kuwa wanadhibiti swala la milipuko ambayo imekuwa ikitokea mara kwa mara na kusababisha athari zikiwemo za kiafya na kuharibika kwa majengo.
Aidha Dr,Medadi Kalemani amewaomba wananchi kuwa wavumilivu na kwamba swala hilo kuanzia jumatatu ya wiki ijayo litafanyiwa kazi na wizara hiyo kwa kupitia mtafiti wa serikali.
Katika hatua nyingine mbunge wa geita mjini Mh Costantine Kanyasu amemshukuru naibu waziri kwa kufika na kujionea namna na jinsi ambavyo wananchi wamekuwa wakiathirika kutokana na milipuko hiyo.
HABARI NA:
JOEL MADUKA
STORMFM GEITA
HABARI NA:
JOEL MADUKA
STORMFM GEITA
Post a Comment