Header Ads

Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli Atembelea Shule ya Msingi Mbuyuni na Kuwaaga Rasmi Walimu Wenzie na Wanafunzi Aliokuwa Akiwafundisha

LEO Feb 17 2016, Mke wa Rais John Pombe Magufuli  Janeth Magufuli amewasili katika shule ya msingi Mbuyuni, Dar  kwa  ajili  ya  kuagana  na  walimu wenzake  pamoja  na  wanafunzi  aliokuwa  akiwafundisha

Shule  ya  Msingi Mbuyuni ni  shule ambayo Mama Magufuli alisoma kuanzia darasa la kwanza na baadaye mwaka 1995 kurudi tena kufundisha hapohapo  kwa miaka 17 hadi mumewe Rais Magufuli  alipochaguliwa  kuwa  Rais  wa  Tanzania.
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akipokea zawadi ya saa toka kwa mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi ya Mbuyuni, Mwalimu Dorothy Mwalecela , Oysterbay, jijini Dar es salaam wakati wa sherehe fupi ya kuwaaga rasmi walimu wenzake na wanafunzi wa shule hiyo
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akisikiliza risala toka kwa mwanafunzi wa shule ya Msingi ya Mbuyuni Oysterbay, jijini Dar es salaam wakati wa sherehe fupi ya kuwaaga rasmi walimu wenzake na wanafunzi wa shule hiyo
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akipokea zawadi toka kwa Afisa Elimu wa Wilaya ya Kinondoni katika Shule ya msingi ya Mbuyuni Oysterbay, jijini Dar es salaam wakati wa sherehe fupi ya kuwaaga rasmi walimu wenzake na wanafunzi wa shule hiyo

Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akisikiliza maelezo ya utangulizi ya mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi ya Mbuyuni, Mwalimu Dorothy Mwalecela , Oysterbay, jijini Dar es salaam wakati wa sherehe fupi ya kuwaaga rasmi walimu wenzake na wanafunzi wa shule hiyo

No comments