WANAODHURUMU WALENGWA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI KUKIONA.
Mratibu wa Tasaf Wilayani Mbogwe mkoani Geita Mercy Joseph amewaonya watendaji ,
mabalozi na wenyeviti wa vijiji na wale
wote wanaofanya mchezo wa kuwadhurumu walengwa wa mpango wa kunusuru kaya
maskini baada ya kupokea msaada huo wao wanawatoza ushuru wakibainika watachukuliwa
hatua kali.
Onyo hilo Mercy amelitoa baada ya Mbunge wa
jimbo la Mbogwe Agustino Masele kuyafikisha malalamiko ya wananchi ofisini
kwake kuwa wapo watu wanaowaomba walengwa fedha
za ushuru kwa kuwa waliwasaidia majina yao kukubaliwa.
Amesema
baada ya kusikia kauli hiyo toka kwa mbuge kuwa kuna watu wanafanya
Mchezo huo
ameamua kupita kila kijiji kuwaelimisha tena walengwa kuwa wasikubali
kumpatia mtu yeyote fedha hizo ambazo wanapokea kila baada ya wiki mbili na
hivyo kama kuna mtu anafanya hivyo huyo ni mwizi hivyo amewataka wamtajie majina ya
watu hao ili awachukulie hatua.
Joyce Peter ni mkazi wa kijiji cha Shinyanga B
amesema kuwa kweli wanafanyiwa hivyo kwa lengo la kwamba waendelee kusaidiwa ili majina yao yasije yakafutwa na kukakosa msaada
Mratibu
wa Tasaf ameongeza kuwa kila anapopita vijijini wananchi wamekuwa
waoga kuwataja wale wanaowafanyia vitendo hivyo kwa kile alichobaini kuwa
huenda wakiwataja basi wanaweza kufanyiwa kitu chochote hivyo ametoa simu yake
kwa walengwa wote waliochaguliwa kwenye uhawilishaji na majina yao yameshaanza
kupokea fedha ili waweze kumtumia majina.
HABARI NA PETER MAKUNGU VIA JOEL MADUKA PEKUZI ZA MTAA.
Post a Comment