Header Ads

Rais Magufuli Ahudhuria Mazishi Ya Kaka Wa Rais Mstaafu Jakaya Kikwete Kijijini Msoga



RAIS John Magufuli jana ameshiriki maziko ya marehemu Selemani Kikwete ambaye ni kaka wa Rais mstaafu, Jakaya Kikwete, yaliyofanyika kijiji cha Msoga, wilaya ya Bagamoyo, mkoani Pwani.

Selemani alifariki dunia Machi mosi, mwaka huu nchini India.

Viongozi wengine waliohudhuria ni Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohammed Shein, Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan na marais wastaafu Ali Hassan Mwinyi na Benjamin Mkapa, Makamu wa Rais mstaafu Dk Mohammed Gharib Bilal, Waziri wa zamani, Shamsi Vuai Nahodha, Waziri Mkuu mstaafu Samuel Malecela na Mufti Abubakary Zuberi.

No comments