Header Ads

CAITLYN JENNER NI MWANAMKE MSHAWISHI.

Caytlin Jenner
Mtu aliyejibadilisha maumbile na kuwa mwanamke Caitlyn Jenner ameorodheshwa miongoni mwa wanawake 10 mashuhuri wenye ushawishi mkubwa pamoja na Angelina Jolie,Singer Sia na Anna Wintour.
Orodha hiyo iliyoongozwa na waziri wa kwanza wa Uskochi Nicola Sturgeon inawatambua wanawake ambao wamekuwa wakiathiri uma pakubwa.
null
Angelina Jolie
Nyota wa kipindi cha Keeping up with the Kardashians Jenner aliyejulikana kama Bruce ameorodheshwa katika nafasi ya saba.
Alibadilisha maumbile yake na kujiita Caitlyn katika jarida la Vanity Fair mwezi uliopita.
null
Nicola Sturgeon
Mwanariadha huyo wa zamani ambaye wanawe ni pamoja na mwana wa kambo Kim Kardashian na Kendall Jenner ametunukiwa heshima ya kuonyesha maumbile yake mapya kwa uma.BBC

No comments